MAOMBI YA MAANDALIZI YA IBADA KUSIFU NA KUABUDU MWISHO WA MWEZI WA AGOSTI 2021

1. KAA MBELE ZA MUNGU KATIKA IBADA NA TOBA 

a) Mwabudu, Msifu na kumshukuru. (Ufunuo 4: 8-11 na Zaburi 89: 1-18). 

b) Weka moyo wako na dhamiri yako sawa kwa njia ya kupokea msamaha wa dhambi. (2 Wakorintho 5: 17-21 na Waefeso 1).

2. KUBALIANA NA ROHO MTAKATIFU ​ 

Kujiombea /idara zote / Watumishi walioalikwa. Chukua muda kutambua kila kitu kizuri kilicho ndani yako katika Kristo Yesu. Filemoni 1: 6.

Amini na umshukuru Mungu:

 • Ambaye hufanya kazi ndani yako kutaka na kutenda kwako ili kulitimiza kusudi lake jema. Wafilipi 2:13 

• Kwamba umeumbwa katika Kristo kufanya matendo mema, ambayo Mungu aliyatengeneza tangu mwanzo ili tuenende nayo. Waefeso 2:10 

• Kwamba ni Mungu mwenyewe anayefanya kazi ndani yako kama alivyofanya katika Kristo. 2 Wakorintho 5: 20-21.

 • Kwamba amekutia mafuta na unajua mambo yote. (1Yohana 2: 20 & 27).

 • Kwamba amekujaza kipimo cha imani kwa ajili ya huduma. Warumi 12: 3-8 

• Kwa sababu unaamini utafanya kazi za Mungu. Yohana 6: 28-29. 

• Kwamba kila atakayehudumu atakuwa na umoja na nia moja. (Yohana 17: 21-23 na Wafilipi 2: 1-2).

• Kwa mwongozo wa Roho Mtakatifu katika kweli yote. Yohana 16: 12-15

3. OMBEA IBADA NZIMA KWA MUJIBU WA NENO: 

• Uwepo wa Mungu ili kutimiza kusudi lake kwa watu wake. 

☆ 1 Wafalme 8: 10-11, Matendo 2: 4 

☆ Marko 16: 17-18 

☆ 2 Wakorintho 3:17 

☆ Yohana 16: 23-24. 

• Neno, Mnenaji wa Neno na Mtafsiri. 

☆ Isaya 50: 4-5 

☆ Waefeso 1: 9-10

• Mahudhurio.

Tangaza kile unachotaka kuona juu ya mahudhurio katika ubora na wingi. 

4. SHUKRANI KWA MUNGU 

Mshukuru Mungu kwa kutimiza ahadi zake kulingana na Zaburi 136. Imba kama Daudi alivyoimba !!!

Join the Discussion

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top